Wednesday, June 21, 2017

IMELETWA KWAKO NA SIMULIZI MIX ENTERTAINMENT
MWANDISHI ZUBERY RAZUUR MAVUGO.
SEHEMU YA NNE                    .

ILIPOISHIA:
   ‘’ Unadhani ni nani? Nd’o huyuhuyu choko aliyetuibia... Kwani nani mwingine.’’ Sauti nyingine ilisikika ikikoroma. Mara ngumi moja ya kichwa ikatua mwilini mwa Maduhu, maumivu yakaandamana na kilio cha nguvu kutoka kwake. Hajakaa sawa, mara akapokea kofi la uso, kutoka katika mkono uliyoshiba kimazoezi. Akiwa katika sintofahau, mara akahisi kama harufu fulani ya damu. Pakepale pua zake mbili zikaanza kutoa damu. Hakupata muda wa kuuliza ama kujiuliza ni kipi alichokosea hadi kipigo kimuangukie?

 ENDELEA... Mtoto yule mwene umri wa miaka saba pekee. Aliinamisha kichwa chake chini na kuruhusu damu kutoka puani imwagike, huku akisahau kuwa wale watu waliyokuwa wamemzunguka hawakuwa wameishia hapo. Akiwa kainamisha kichwa mara kofi jingine likatua katika uso wake kwa mara nyingine pasina kuhofia damu zilizokuwa zikimtoka mtoto yule. Hapo maumivu yakamzidi, akawaza nini afanye? Na vipi anakutana na kipigo namna ile utadhani ameikosea dunia. Wakati akijiuliza, mara ikasikika sauti ya kike.

      ‘’ Jamani, ni bora tumpeleke moja kwa moja kituoni huyu mtoto, itakuwaje atuibie pesa zote za sherehe?’’ Ha! Hapo mwili mzima wa mtoto yule ukamsisimka, hofu ikamjaa huku akiwaza jambo lile jipya alilofikishiwa, ati kapora pesa za sherehe! Saa ngapi? Hata hivyo, makelele ya waliyomzunguka hayakuweza kumpatia hata muda wa kujiwazia. Ni wazi, waliyomzunguka walikuwa na hasira sana, mmoja kati yao alimbebelea kwa mikono miwili na bila huruma akamtupa kwa nguvu chini na kumsababishia mtoto yule atoe ukelele mkali. Kisha wakamchukuwa mzobemzobe na safari ya kuanza kumpeleka kituoni ikaanza.

  Wakati huo, hakuna ambaye hakutaka kuamini kuwa mtoto yule si mwizi. Kila mmoja aliamini kuwa, hakuna aliyeiba isipokuwa yeye maana hata wakati pesa zile zinaibiwa, mwizi alikuwa amevalia mavazi machafu ya kichokoraa kama yeye huku hata umri wakiwa wanaendana. Hatimae walimfikisha kituoni.

Huko kituoni pia hakukuwa na msalie mtume. Kipigo cha mbwa mwizi kilimwangukia kama hana akili vizuri huku aking’ang’anizwa aweze kukili kuiba pesa zile ambazo hata hazifahamu na wala hafahamu ninani aliyeziiba. Adhabu mbalimbali alipatiwa tena bila kuhurumiwa, alipokili kuumizwa na adhabu zile, waadhibu hawakumwacha waliendelea kumuadhibu haswa! Huku wakimlazimisha akubali kuwa, yeye nd’o mtu aliyeziiba pesa zile.

Ingawa alikuwa mtoto mdogo lakini hakuwa mjinga kiasi cha kukubali jambo lisilomuhusu.

   Adhabu zilimpelekea kupoteza hadi fahamu, akawa hajitambui na wala hatambui kilichokuwa kikiendelea.

 Muda wote huo wa adhabu, wale waliyomleta tayari walikuwa wameshaondoka zamani sana. Lakini baada ya muda kupita walirejea kwa mara nyingine kituoni huku wakiwa na mtoto mwingine aliyevalia kama yeye.

 ‘’ Afande, tunaomba mtuwie radhi... Huyo mtoto aliyemo ndani hana hatia, mwenye hatia ni huyu hapa.’’ Mwanaume mmoja aliyeonekana na sura ya ghadhabu alisema maneno yale.

   ‘’ Kwahiyo, mnataka kusema yule hahusiki na lolote? Mbona amekaa kama kibaka tu?’’

    ‘’ Ndivyo afande. Mwizi ni huyu hapa, tumembamba sehemu, yule mtoto tulimfananiha tu.’’ Bwana mwingine alisema huku yeye akiongeza kwa kumpiga makone kadhaa mtoto ambaye walikuwa wameshikilia.

 Kituoni hakuna maswala ya kuuliza, walimchukuwa mtoto mwingine aliyeletwa pale ambaye kiasi fulani yeye alionekana kuwa nunda maana alijaribu hadi kuwabishia wao. Hapo afande mmoja akaamua kumuonesha kazi ya rungu. Mtoto yule hakukubali kuyastahimili maumivu aliyoyapata, kwa hasira akajibu mashambulizi kwa kumrushia kichwa afande aliyehusika kumpiga rungu lile. Akawa amechokoza nyoka bila mweyewe kujitambua. Hapo ndipo alipokipata cha mtema kuni.

  Maduhu alipozinduka alishangaa sana baada ya kuona hajafungwa pingu mikononi na wala hayupo ndani ya kile chumb cha mateso.  Hata baada ya kuonduka, wale waliyomleta kituoni walichukuwa jukumu la kweda kumtibisha huku wakimwomba msamaha.

  Alikaa hospitali kwa muda wa siku tatu kutokana na majiraha aliyokuwanayo. Kuna wakati alikuwa akikumbuka mbali sana, kipindicha nyuma.

    ***

‘’ Mdogo wangu, najua unajuawazi kuwa, maisha yetu ni magumu na hiyo ni sababu hata ya sisi kutokusoma, ila usijali... Mimi nitatafuta pesa kuhakikisha wewe siku moja unaingia darasani.’’

 ‘’ Nimekuelewa kaka. Lakini, kwanini sisi tunasemwa vibaya, iwe nyumbani? Iwe shuleni.’’

  ‘’ Ni kwasababu sisi hatuna pesa. Ila ipo siku watatuheshimu tu... Futa machozi mdogo wangu.’’

***

 Kumbukumbu zile ziliambatana na kilio. Hakutaka kuamini kama wazazi wake pamoja na kaka yake hawapo tena ndani ya dunia hiyo. Akifikiria ni wapi ataelekea? Ni kweli kabisa, historia ya baba yake haikuwa na mantiki sana. Inasemekana kuwa, baada ya kuhamia ndani ya jiji hilo ambalo kwalo ndiko alianza maisha mapya, alitoka katika mji mmoja ambao upo mkoa wa mbali sana na jiji hilo, hakuhitaji tena kurejea nyumbani kwao ingawa hakikujulikana kisa cha yeye kutokuhitaji kurejea huko. Hata alipofika katika jiji hilo alilofia, alikutana na mwanamke mmoja ambaye naye pia ni marehemu; mama yule alikuwa akifanya kazi za ndani huku maisha yake pia yakiwa hayana mbele wala nyuma. Wakapendana, mpenzi yao yakafika mbali zaidi hadi wkajikuta kwa bahati mbaya mimba inamuingia mwanamke yule. Hapo ikawa kasheshe. Akatimuliwa kule alipokuwa akifanyia kazi, ndipo hapo alipoanza kuishi rasimi na manaume yule. Ingawa mwanzoni maisha yao yalikuwa ya kawaida lakini kuzaliwa kwa watoto kidogo kulikuja na mabalaa. Kipato kikashuka wakashindwa hata kuwa wakijikimu, wimbi la umasikini likawavaa haswahaswa bila utani.

   Nguo wakawa wakivaliana, baba akiwarithisha hadi wanae nguo zake. Mawazo mengi sana kuhusu familia, yalimpelekea mzee yule akijikute akikumbwa na ugonjwa usiyojulikana. Na huo nd’o ugonjwa ulliyomtwaa. Huku akionmdoka na roho ya mkewe pamoja na ,mwanae, wakamwacha mtoto mogo mwenye umri wa miaka saba. Asiyejua mbele wai wala nyuma wapi.

  Mtoto yule yatima, tayari mateso ya kuwa mbali na wazazi yalianza kumpata. Akaanza kugundua kumbe ukiwa yatima huthaminiwi, ukiwa fukara huangaliwi. Watui wapo radhi wakuondoe hata kwenye ulimwengu. Akiwa bado katika tafakari nzito huku bado ruhusa kutoka kwa daktari haijamfika. Alijikuta akipandwa na uchungu.

    ‘’ Wazazi wangu... Kwanini lakini mmeondoka? Kwanini mmeniacha katika mateso haya? Tazama, simtambui ndugu yeyote kutoka kwa baba wala kwa mama. Ni vipi nitaweza kuishi ndani ya dunia hii? Dunia isiyenithamini wala isiyo nihurumia? Wazazi, ikiwa ninyi ndio tegemeo langu kuu na mmeniacha, mnadhani nitakuwaje? Ona, ninateswa bila hata kosa...’’ Alilalamika sana, lakini hakuna kilichobadilika, zaidi ni badliko la sura pekee. Uso ukitengeneza tabasamu la kununa huku machozi yakimmiminika.

  Muda kidogo, daktari aliingia ndani mule na kumwita nmtoto yule hospitali kisha akamweleza kuwa, angependa kumruhusu aweze kwenda maana tayari hali yake ilikuwa nzuri.

   ‘’ Dokta, samahani sana... Wewe ni kama baba yangu, na ninaimani unawatoto kama mimi. Tafadhali naomba uniachie niendelee walau kuishi hapahapa hospitali, huko nje sipawezi mimi. Wazazi wangu wamefariki, sijui hata wapi nielekee. Sina ndugu wala jamaa yeyote katika hii dunia.’’ Mtoto yule aliongea hayo kwa uchungu baada ya kuwa amepewa ruhusa ya kuondoka hospitali pale.

  Daktari akamtazama mtoto yule kwa jicho la huruma utadhani mtu mwenye kuhitaji kumsaidia kisha akasema,

‘’Hospitali ni sehemu ya wagonjwa tu na si watu wazima. Hata hivyo, unaonekana kijana mdogo sana ambaye bado matatizo hujayazoea. Ni watoto wengi na hata wakubwa wenye matatizo tena zaidi yako wanakuja hapa na kuomba kama unavyoomba wewe, lakini tunashindwa jinsi ya kuwasaidia. Labda nikusaidie kwa kusema. Mwanaume wa kweli huwa hayaogopi matatizo, nenda hukohuko yalipo ili uweze kukuwa ki akili na kutengemaa kifikra, sisi pia tumepitia magumu, na kupitia hayo tumejifunza na kuwa hapa tulipo leo.’’


      ITAENDELEA.

0 comments:

Post a Comment