Wednesday, June 14, 2017

IMELETWA KWAKO NA: SIMULIZIMIX ENTERTAINMENT.
MWANDISHI: FRANK MASAI.
                         UTANGULIZI.
     Ni katika nchi ya Tanzania nchi inayo aminika kua na utajiri mkubwa sana ingawaje asilimia kubwa ya wananchi wake ni masikini, kuna sehemu mwandishi anauliza inawezekanaje wananchi wakawa matajiri wakati wengi wa viongozi wanajali matumbo yao kwanza ambayo hata hayajai…. Na ni ndani ya nchi hiyo hiyo inayosemekana ni nchi ya kidemocrasia lakini bado mwandishi akauliza utasemaje ni nchi ya democrasia wakati ukitaka kusema unazimwa, wala mwandishi hakutaka kuyazungumzia hayo katika simulizi hii alichosema ni kua embu taachane na hayo maana haya husiki katika simulizi hii ila yanayo husika katika simulizi hii ni haya.

DUKA LA ROHO ni kikosi kinachoendesha matendo ya kigaidi ndani ya nchi ya Tanzania huku wakidai kua kazi yao kubwa ni kuuza na kununua roho za watu… Yani kama ukiingilia mipango yao basi unakua umeiweka roho yako au roho za uwapendao dukani ambapo itakubidi uinunue roho yako au roho za uwapendao kwa kufanya kile watakacho kitaka wao au uuze roho yako au za uwapendao kwa kutotii kile walicho kutaka wewe ukifanye..  kwa kufanya hivyo viongozi wengi ambao wanafanya kazi kwa kufuata sharia wanaondolewa duniani na wengine wanalazimishwa kujiuzuru kutoka katika nyazifa mbali mbali ili kuzinunua roho zao au za wawapendao baada ya kua zimewekwa dukani na kikosi hiki cha duka la roho.

Mbaya Zaidi ni kua raisi wa nchi hiyo ya Tanzania nae roho yake imewekwa dukani hivyo anaendeshwa na kikundi hicho cha DUKA LA ROHO jambo linalomfanya afanye maamuzi ya ajabu yanayoshangaza wananchi wake ikiwemo kuwafukuza kazi viongozi na wanausalama wanaofanya kazi kwa kufata haki na sharia ya nchi na kuwateua viongozi na wanausalama ambao ni vibaraka wa DUKA LA ROHO ambao wanafanya kazi kwa kufata matakwa ya kikosi hicho na si haki ya wananchi.

Lakini anakuepo kijana mmoja ambae ni mtanzania halisi  mwenye uwezo mkubwa wa kupigana iwe ni kwa kutumia siraha au mapigano ya ana kwa ana basi ukiingia katika anga za huyo kijana basi hutoki…. Kubwa kuliko yote ni uwezo wake mkubwa katika mambo ya sayansi na technolojia…. Aliwahi kusomea chuo cha sayansi nchini china na akawa ni moja kati ya wanasayansi sita walio wahi kutengeneza mtambo mmoja uitwao SGT wenye uwezo mkubwa sana duniani na wenye uwezo wa kufanya kazi nyingi sana za kipelelezi…. Ikiwemo uwezo wa kuzima satellite zote duniani na aina zote za mawasiliano na kuweza kuiba siri za nchi za nchi yoyote

Wakati kikundi hiki cha duka la roho kinashamili kuendesha matendo ya kigaidi nchini Tanzania kijana huyu alikua mafichoni nchi za mbali hii ni kutokana na kua anatafutwa sana na afisa usalama wa Tanzania tu, bali pia anatafutwa vikali na shirika la kipelelezi la marekani FBI hii ni kutokana na matukio makubwa aliyowahi kuyafanya huko nyuma kwa kutumia uwezo wake wa kisayansi ikiwepo kuiba kwa kutumia technologia…. FBI wanamtafta sana wanashindwa kumpata yote hayo ni kwa sababu ya uwezo wake wa kucheza na technoloji kwa kuzuia aina yoyote ya vifaa vya kipelelezi vinavyoweza kung’amua ni wapi alipo.

Baada ya maovu ya kikudi cha DUKA LA ROHO kuzidi mbaya Zaidi kufikia sehemu ambayo wanaiweka dukani roho ya mtoto wa kijana huyo ambaye ndo yuko mafichoni nchi za mbali kwa kumpa masaa 24 mama wa mtoto huyo ambae ni mwanamke aliyezaa na kijana huyo kuweza kujipeleka mwenyewe  mikononi mwa kikundi hicho ili kuweza kununua roho ya mwanae kwa kuiuza roho yake. Na hii ni baada ya kwenda kinyume na mipango ya kikosi hicho cha duka la roho… Lakini kijana yule alie mafichoni anapata kunasa mpango mzima wa kikosi hicho hivyo anafunga safari kutoka huko mafichoni kwa lengo moja tu kuja kuiokoa familia yake.
Anafanikiwa kuzuia mpango wa kikosi cha DUKA LA ROHO wa kuiteketeza familia yake lakini pia anafanikiwa kuzuia mashambulizi mengi ya kigaidi yaliyokua yamepangwa kufanywa na kikosi hicho  ndani ya nchi ya Tanzania yote hayo anayafanya kwa kutumia uwezo wake mkubwa wa kucheza na sayansi na technolojia lakini pia kwa uwezo wake wa mapigano ya ana kwa ana.

Kwa kutambau uwezo wa kijana huyo kikosi cha Duka la roho kinatafuta kila njia ya kumuangamiza wanashindwa…. Mpaka wanatumwa wauwaji wa kimataifa wa kizungu “Pro killers” ambao hawajawahi shindwa mission yoyote  na wameuwa watu wengi sana ili kwa mikono ya kijana huyo wanajikuta wakiuliwa wao… Hapo ndo kikundi cha DUKA LA ROHO kinaona njia pekee ya kumnasa kijana huyo ni kuishinikiza serekali iweze kumtafuta na kumkabizisha kwao ila kiukweli hata serikali yenyewe haina jinsi ya kumkamata kijana huyo… Kikundi hicho bila kujali kua hata serikali haiwezi kumkamata kijana huyo chenyewe kinaanza kuendesha mauaji ya askari popote askari atakapoonekana wenyewe ni wanaua wakidai mauaji hayo yatakoma mara tu serikali itakapo wakabidhi kijana huyo…

Baada ya mauaji ya askari kuzidi kijana huyo anawasiliana na raisi wa nchi na raisi kwa kutambua uwezo wa kijana huyo anamuomba kijana huyo waungane ili kuweza kuteketeza kikosi hicho cha DUKA LA ROHO ingawa rahisi anajua fika kijana huyo anatafutwa kila kona  sio na Tanzania tu bali pia na shirika la kipelelezi la marekani FBI. Makubaliano yanapitishwa na raisi anamkabidhi kijana huyo siraha zote alizo zihitaji kwa lengo la kuteketeza kabisa kikundi cha duka la roho.
Kijana huyo akiwa na kikosi kidogo cha wanausalama ambao walifukuzwa kazi na raisi baada ya kuanza kufatilia kikundi hicho cha DUKA LA ROHO..... Je wataweza kufanikiwa kukiteketeza kikosi hicho? 

KUSOMA SEHEMU YA KWANZA BOFYA HAPA DUKA LA ROHO 01

UNAWEZAJE SASA KUKOSA KUFATILIA HADITHI HII NZURI YA MAPIGANO? HADITHI ILIYOPANGILIWA MATUKIO NA MWANDISHI WETU KWA JINSI AMBAYO ITAWEZA KUKUBURUDISHA, KUKUSISIMUA NA KUKUELIMISHA… HIVYO USIKOSE KUFATILIA HADITHI HII KUJUA KIJANA HUYO WA KITANZANIA MWENYE UWEZO MKUBWA WA KISAYANSI, MAPIGANO YA KIVITA NA MAPIGANO YA ANA KWA ANA, NI NANI? NA NI YAPI MAKUBWA YA KUFURAHISHA NA KUSHANGAZA ALIYOYAFANYA NDANI YA SIMULIZI HII… HAKIKA UTAFURAHI NA KUBURUDIKA KWA KAZI ZAKE MWANANA ALIZO ZIFANYA NDANI YA HADITHI  HII…. PIA UTAWEZA KUJUA NI WATU GANI WANAOKIENDESHA KIKOSI HICHO CHA DUKA LA ROHO PIA UTATAMBUA UWEZO WAO WA KUTISHA KATIKA KUZIFANYA KAZI ZAO JAPO PAMOJA NA UWEZO WAO HAWAKUWEZA KUPITA KATIKA MIKONO YA KIJANA WETU MASHUHULI.. USIKOSE NA UNGANA NA  SIMULIZI MIX ENTERTAINMENT AMBAO WATAKULETEA KISA HIKI MWANZO MPAKA MWISHO…  SALUTI KWA FRANK MASAI AMBAE YEYE NDO MTUNZI NA MWANDISHI WA HADITHI HII. JAMAA MMOJA ANAFANYA KAZI ZAKE VIZURI SANA NA UTAUSOMA UWEZO WAKE KUPITIA HADITHI HII

KUSOMA SEHEMU YA KWANZA BOFYA HAPA DUKA LA ROHO 01

UTAPATA HADITHI HII  NA NYINGINE NYINGI ZITAKAZOLETWA KWAKO NA SIMULIZI MIX ENTERTAINMENT KATIKA BLOG www.simulizimix.com FACEBOOK, INTAGRAM NA TWITTER @simulizimix .. YOUTUBE Simulizi Mix Entertainment WHATSAPP 0712505163 ... TUMA NENO GROUP KUONGEZWA KWENYE MAGRUP YA SIMULIZI MIX ENTERTAINMENT AU TUMA NENO INBOX KUPATA SIMULIZI ZETU INBOX YA SIMU YAKO., UKITUMA NENO INBOX HAKIKISHA UMASAVE NAMBA YETU KWENYE SIMU YAKO.

SHARING IS CARING, USISAHAU KUCOMENT LAKINI PIA KUSHARE HADITHI ZETU KWAUWAPENDAO NDUGU JAMAA NA MARAFIKI ILI UWEZE KUBURUDIKA NA KUELIMIKA PAMOJA NAO.

SIMULIZI MIX ENTERTAINMENT WE TOUCH YOUR FEELINGS


0 comments:

Post a Comment