Tuesday, June 20, 2017

IMELETWA KWAKO NA SIMULIZ MIX ENTERTAINMENT
MWANDISHI NI FRANK MASAI
SEHEMU YA PILI

ILIPOISHIA
"Ooooh! Ni Prince Mubarak." Jamaa yule aliongea baada ya kujifuta damu zilizokuwa zinamchuruzika. "Na swali.moja tu kwako, na usipolijibu, nitakupa onyo tu." Jamaa alimtazama Mubah kabla hajauliza swali lake. "Kwa nini umeamua kuweka dukani roho za uwapendao?" Jamaa alimuuliza Mubah lakini badala ya Mubah kujibu, yeye akachukua gundi aina ya 'sole tape' na kuizungusha mdomoni mwa mtuhumiwa yule mwenye mdomo wa kero na kukereketa.
"Thats will help, I think. (Hiyo itasaidia nadhani)" Lisa aliongea akikubaliana na kitendo kilichofanywa na Mubah.
ENDELEA
 **** Safari yao ilikomea eneo moja la ufukwe wa bahari ya hindi. Na baada ya hapo, Lisa alitoa simu yake ya mkononi na kuipiga.  Maongezi yalichukua dakika chache na simu ikakatwa.
Baada ya dakika zisizozidi kumi za kukata simu ile, kwa mbali, kwa kutumia darubini yake, Lisa aliona Nyambizi ikiibuka toka chini ya bahari na baadae ikafunguka kwa juu na boti ndogo saba zikatoka ndani yake. Boti hizo ni zile ziwezazo kubeba watu wawili kila boti moja.  Waendeshaji walikuwa wamevalia mavazi ya kuogolea na bunduki aina M16 zikiwa migongoni mwao. Lisa akashushia darubini yake kifuani na kuwapa ishara wenzake ya kujiandaa hasa kutoka mle garini.
Boti saba zikasimama mbele ya wakubwa wa kazi, na kitendo bila kuchelewa, kundi linaloongozwa na Lisa likiwa na mtuhumiwa wao, wakakwea nyuma ya boti hizo ndogo na safari fupi ya kwenda kwenye Nyambizi moja ndogo kiasi, ikaanza.
Boti tano zikiwa mbele na nyingine mbili nyuma zikilinda usalama ili yule mtuhumiwa asitoroke, zikazidi kukata maji kuelekea kwenye nyambizi. Wakiwa katika umbali fulani, Lisa alimuamuru dereva wa boti yake asimame. Naye baada ya kusimama, Lisa aligeuka nyuma na kuangalia kule alipotoka.
Kulikuwa hakuna watu wanaozunguka eneo lile, hiyo ikawa nafasi pekee ya Lisa kufanya alichokusudia.
Akatoa rimoti ndogo ambayo alibofya kitufe kimoja kilichokuwepo katikati. Na hapohapo, mlipuko mkubwa uliikumba ardhi ambayo gari aina ya Noah ilikuwa imeweka makao kwa muda.  Ni ile gari ambayo walikuwa wanaitumia Lisa na kundi lake. Baada ya kumalizia kazi ambayo waliipanga, sasa waliiteketeza na kuacha Jiji dogo la Dar Es Salaam kutetemeka kwa huo mlipuko. Wafanyakazi wa maeneo yale walikimbia huku na huko wakihisi jiji limevamiwa na magaidi hatari. Hakuna aliyekumbuka kugeuka nyuma, wote walikuwa wakinusuru roho zao. Hakika ilikuwa ni mshike mshike maeneo yale.
Baada ya kulidhika na kazi yake, Lisa akamgonga bega kumruhusu dereva wake aondoke, naye akatii amri na kwenda sehemu ambayo walipanga waende. **** Ndani ya nyambizi ile, kulikuwa kuna pilika za hapa na pale hasa wale mafundi mitambo wanaongoza chombo kile maalumu kwa ajili ya kazi za kijeshi au kiusalama. Naam, baada ya Lisa na kundi lake wakiwa sambamba na mtuhumiwa wao kuingia kwenye chombo kile, waliongozwa kwenye chumba maalumu na kuoneshwa nafasi zao za kukaa.  Baada ya kukaa, alitokea daktari mmoja akiongozana na kijana aliyebeba sinia dogo lililokuwa na sindano uwezazo kuzikamata kama bastola. Sindano hizo zenye dawa kiasi, kila mmoja alichomwa begani na baada ya dakika chache, macho ya hawa watu yakaanza kuwa mazito.
"Kazi za utumwa hizi. Hamtakiwi kujua hata ni wapi mnafanyia kazi na ndio maana mnapigwa sindano za usingizi ili msione mnapoenda. Stupid peoples." Sauti nzito iliyochanganyanyika na ulevi, ilimtoka yule mtuhumiwa aliyekuwa huru kuongea baada ya kutolewa ile gundi aliyozungushiwa na Mubah. Hakuna aliyemjibu na badala yake, kila mmoja alibebwa na usingizi mzito. ****
FISSA (Federal Intelligence Secret Service Agencies)
Mlango mmoja mkubwa uliandikwa maandishi hayo ambapo ndipo hasa Lisa na Mubah wanafanya kazi zao. Ule usingizi mrefu ulikuwa umewapaa na sasa walikuwa wanatembea wenyewe huku wakimkwida vema mtuhumiwa wao ili asiwaponyoke.
"Kazi nzuri Agent Lisa. Mmefanya vizuri na kikosi chako." Sauti ya mtu mmoja mrefu kiasi na mweusi, ilisikika ikiwa kwenye jukwaa dogo ambalo mbele yake kulikuwa na watu wanachakalika na kompyuta zao huku skrini moja kubwa ikionesha kazi nzima wafanyazo wale wafanyakazi.
"Asante mkuu." Lisa alishukuru huku akiinama kidogo kuonesha heshima kwa mkuu wake wa kazi. Mkuu yule akashuka toka kwenye lile jukwaa na moja kwa moja akamfuata yule mtuhumiwa na kumuangalia kwa macho makali kabla hajaanza kuongea.
"John Lobo. Nilishangaa sana nilipoambiwa kuwa u mzima. Nilikuua kwa mikono yangu, lakini leo ni kama nakutana na mzimu." Sauti ya yule bwana ilipenyeza kwenye masikio ya kila mmoja aliyesikia vema maongezi yale. "Sina kesi na wewe. Nilishakuua kipindi kile, hapa naanza na kesi nyingine." Alimaliza Mkuu wa FISSA na kugeuka nyuma kurudi kwenye lile jukwaa dogo.
"Malocha Malingumu." Sauti ya John Lobo, mtuhumiwa aliyekamatwa na kundi la Lisa, ilimuita yule mkuu wa kitengo cha siri cha huduma za kipelelezi nchini Tanzania. Bwana Malocha akasimama kumsikiliza kimtokacho John Lobo. "Siyo kosa langu kuua familia yako. Nilinunua roho zao kwa kuamrishwa na shetani langu. Usilalamike sana. Hahahahahaaa." Lobo alimaliza kwa cheko lake la kukera kushinda hata la katuni au fisi.
"Mpelekeni Hell in Hell." Malocha akaamuru na kila mmoja alishituka baada ya kusikia amri hiyo. "Hamjanisikia?" Malocha aliuliza baada ya kuona hakuna kinachotendeka baada ya amri.
"Lakini Mkuu huyu tutampoteza kule. Kumbuka CIA na FBi wanamtaka mzima." Lisa akiongea kumuelewesha mkuu wake.
"Kwa hiyo unashauri apelekwe wapi?" Malocha akauliza tena swali.
"Nadhani twende naye 123K." Alitoa wazo Lisa.
"Kwa hiyo akakae tu! Kaja kukaa hapa au kusema ukweli?" Malocha alimtupia swali Lisa.
"Lakini si kumpeleka Hell in Hell. Atasema nini kule?" Lisa alijitetea.
"Hivi mmenileta huku nije kusema kitu au nije kupiga story na 'school mate' wenzangu?" Lobo alifungua kinywa chake na kuwauliza wale wanaoshauriana wapi wampeleke. "Kama mnataka mnijue au niseme chochote, hilo mmekosea. Hapa hampati kitu wajinga nyie." Lobo akamaliza na hapohapo ngumi nzito ya tumbo ilitua. Alikuwa ni Mubah aliyemuadabisha.
"Utalipa hii dogo." Lobo alimwambia Mubah na Mubah badala ya kutilia maanani yale maneno, alimuongeza konde lingine zito la tumboni.
"Big Mistake(Kosa kubwa) Lakini bado unanafasi ya kulisawazisha." Lobo alimwambia tena Mubah baada ya kuinuka alipokuwa kainama kwa sababu ya kupigwa ngumi ile.
"Mpelekeni 123F6."Malocha aliamuru tena. Na kitendo bila kuchelewa, Lisa na Mubarak walimkamata kushoto na kulia na kuanza kumkokota kwenda chumba walichokiita 123F6.

HELL IN HELL

Hichi ni chumba kipana kilichopo ndani ya FISSA. Ndani ya chumba hiki kuna kiti cha umeme ambacho hutumika kuwasulubu watuhumiwa nguri na saa nyingine kuwaua.
Pia kuna tank kubwa ambalo limejengwa kwa vioo, na tank hilo ndani yake kuna maji. Pia hutumika kusulubisha watuhumiwa kwa kuwazamisha humo au wakiona haongei, hufungulia umeme uliyoungwa ndani ya tank hilo na kuanza kumpiga shoti mtuhumiwa. Hizo ni silaha chache zilizopo katika chumba kiitwacho Hell In Hell. Mbali na hayo, kuna vifaa vya kunyongea na kuchania ngozi.  Ni chumba ambacho kinaogopwa hata na wafanyakazi wenyewe. Kinatisha kwa matendo yanayofanyika huko.

123K
Hiki pia ni chumba kilichopo hukohuko FISSA. Chumba hiki pia ni kipana na kina meza moja kubwa pamoja na kioo ambacho ukiwa ndani huwezi kumuona wa nje lakini wa nje anamuona wa ndani. Chumba hichi ni kwa ajili ya kumuhoji mtuhumiwa kwa mdomo bila kumsulubisha. Na hata kama watataka.kufanya hivyo, basi hutumia viungo vyao kama ngumi na mateke.

123F6
Hiki ni chumba kipana pia kwa ajili ya mahojiano na watuhumiwa. Ndani ya chumba hiki, mahojiano huwa ni ya kulazimisha uongee ukweli kwa kubanwa na silaha mbalimbali pamoja kuchomwa na vitu vyenye ncha kali lakini lengo likiwa utoke mzima.  Na mara nyingi kama mtuhumiwa ni mgumu, basi hupigwa sindano yenye dawa kali ambayo hufanya ubongo na akili ya mtuhumiwa iwaze kusema ukweli tu.
Humo ndimo ambamo John Lobo kapelekwa. Nyuso mbili ambazo hazina utani zilikuwa zimesimama pembeni ya chumba hicho huku wakijaribu jaribu vifaa vyao. Mzee mmoja ambaye alikuwa anapuliza gesi yenye moto juu, aligeuka haraka baada ya kusikia mlango wa chumba kile ukifunguliwa.
"Ooh! Lisa. Umefanikiwa kumkamata Lobo. Kazi nzuri sana binti." Mzee yule aliongea kumpongeza Lisa.
"Asante Babu Pujini, hakuleta shida wakati wa kumkamata." Lisa alimjibu Mzee Pujini ambaye alikuwa ana asili fulani ya Kihindi lakini ni Muafrika halisi kutoka Tanzania.
"Good Lisa. Ndio umemleta kwenye shughuli eeh." Mzee Pujini aliongea huku akianza kuchezea tena ile gesi kwenye kibubu maalumu kinachotengeneza moto huo wa gesi.
"Ndio babu. Fanya yako." Lisa alijibu na wakati huo Mubah alikuwa anafungua pingu alizokuwa kamfunga John Lobo.
Licha ya Lisa na Mzee Pujini kuongea mengi yanayomhusu John Lobo, lakini Lobo mwenyewe hakuwepo kwenye dunia yao bali macho yake yalikuwa yakipepesa huku na huko, chini na juu ya chumba kile.
"Huyu hapa Mzee." Sauti ya Mubarak ilisikika huku ikifuatiwa na kumsukuma Lobo kwa mzee yule bingwa wa kutoa adhabu kwa watuhumiwa mbalimbali.
"Beda. Muondoe misuti yake huyu bwana." Mzee Pujini alimsukumia Lobo kwa Beda, jamaa fulani wa makamo na kwenye mwili mkubwa kutokana na kunyanyua vitu vizito.

Naye Beda bila kuchelewa, akaanza kumwondoa nguo John Lobo na wakati huo Lisa na Mubah walishatoka katika chumba kile na Mzee Pujini alishakifunga. 

ITAENDELEA 

JE NI MATESO GANI ALIYAPATA KIJANA ROBO? BOFYA HAPA>> SEHEMU  YA TATU KUJUA NI NINI KILITOKEA

0 comments:

Post a Comment