IMELETWA KWAKO NA SIMULIZI MIX ENTERTAINMENT
MWANDISHI ZUBERY RAZUUR MAVUGO.
SEHEMU YA TANO.
ILIPOISHIA:
‘’Hospitali ni sehemu ya wagonjwa tu na si
watu wazima. Hata hivyo, unaonekana kijana mdogo sana ambaye bado matatizo
hujayazoea. Ni watoto wengi na hata wakubwa wenye matatizo tena zaidi yako
wanakuja hapa na kuomba kama unavyoomba wewe, lakini tunashindwa jinsi ya
kuwasaidia. Labda nikusaidie kwa kusema. Mwanaume wa kweli huwa hayaogopi
matatizo, nenda hukohuko yalipo ili uweze kukuwa ki akili na kutengemaa
kifikra, sisi pia tumepitia magumu, na kupitia hayo tumejifunza na kuwa hapa
tulipo leo.’’
ENDELEA... Hayo nd’o
yalikuwa majibu ya Daktari; majibu ambayokwa kiasi fulani yaliweza kummaliza
kabisa nguvu mtoto yule.
Mtoto
yule mchafu kwa jina la Maduhu alibaki amechoka huku pumzi ya kukata tamaa
ikimtoka. Akakosa jinsi. Akaona eneo lile kwake si sahihi. Taratibu akaichukuwa
miguu yake na kuanza safari ya kuondoka huku mikono yake kaiweka juu ya kichwa
chake kuashiria jinsi ambavyo mambo yamemzidi.
Wakati akiwa njiani, kichwa chake kilikuwa na
wingi wa mawazo haswa. Hakupanda daladala ingawa zilikuwepo nyingi sana jijini
pale. Aliiamini miguu yake hivyo alikuwa akitembea tu. Kuna wakati alijikuta
akikoswakoswa mpaka na magari kutokana na wingi wa mawazo.
Kwanini
watu hawanahuruma? Ina maana huyo daktari hana watoto? Mbona ananifanyia hivyo
mimi? Kipi ambacho nimemkosea hadi kunifaradhishia matatizo katika maisha
yangu. Kwanini lakini inakuwa hivi, kwanini? Sina pakwenda, wapi nielekee?
Maneno yale yalitembea ndani ya kichwa cha yule mtoto. Akiwa njiani peke yake
aliendelea kuikata mitaa mbalimbali ya jiji hilo la Mwanza. Kama kawaida
alijishauri aelekee angalau nyumbani alipokuwa akiishi na wazazi wake maana
nyumba ilikuwepo. Kwakuwa nyumbani kwao hapa kuwa mbali sana, hivyo
haikumchukuwa muda sana kufika.
Hata alipofika, hakuna ambacho alikiona cha
muhimu kufanya. Nyumba ilimtisha huku kila akiwa ndani kumbukumbu za wazazi
wake zikimwijia. Mawazo ya kitoto yakizidi kumrubuni, huku mengine
yakimhakikishia kuwa, endapo ataendelea kukaa eneo lile, basi mizimu ya wazazi
wake itamwijia na kumchukuwa maana ni yeye tu aliyebaki duniani.
Kuna wakati
alihisi jambo lile ni hofu yake binafsi anayojiwekea ndani ya akili zake.
‘’ Mimi ni mtoto wa kiume.. Siogopi chochote.’’ Alijitia
matumaini kisha akakiendea kitanda kwa ajili ya kwenda kujipumzisha maana
alikuwa amechoka sana. Akiwa juu ya kitanda, usingizi ulimchukuwa. Hapo
hakuelewa tena chochote kilichokuwa kikiendelea ndani ya dunia hii.
Masaa kadhaa baadae
aliamka. Haja kaa sawa tumbo
likamuunguruma kumuonesha kuwa alikuwa na njaa kali.
‘’ Ah! Ndani hamna
chochote, sasa nitakula vipi mie?’’ Alisema huku akiendelea kufunua masufuria
na macho yake yakiangaza huku na kule ndani ya nyumba yao, lakini hakuna
alichoambulia.
Akaendelea
kutafakari jinsi gani anaweza kupata chakula. Hisia za mtembea bure si sawa na
mkaa bure zikamwijia mtoto yule. Hapo akatamani kutoka nyumbani kwao na kwenda
kutafuta chochote kitachomwezesha kukidhi haja ya tumbo lake.
Aliliendea genge
moja lililopo karibu na nyumbani kwao. Akamkuta mamantilie akiendelea na kazi
za upishi. Akamsalimu mamantilie wa genge lile na baada ya hapo aliagiza
chakula alichohitaji. Naam, alikuwa na kiburi cha mchango aliyochangiwa na
wasamalia wema waliyohudhuria mazishini, hata hivyo mchango ule haukuwa mwingi
lakini ulimtosha kuyaendesha maisha yake kwa siku kadhaa.
Hata alipomaliza
kupata chakula, akajichanganya mitaani, huko alisurura mpaka majira ya usiku
yalipofika. Hapo akarejea nyumbani kwake kwa ajili ya kulala.
Maisha mapya ya
kujitegemea akayaanza mtoto yule. Akawa yeye nd’o baba, yeye nd’o mama.
Siku zikaanza
kwenda. Hata hivyo, pesa alizokuwanazo pia hazikuchukuwa hata wiki, zikawa zote
zimemwishia.
Kila alipojaribu
kwenda kuomba msaada, hakuupata. Njaa ikawa rafiki yake kipenzi, haikuhitaji
kumtenga wala kumsahau kila muda ilikuwanaye. Mtoto yule wa miaka saba pekee,
maji yalimfika shingoni, akakitazama kile kibanda ambacho ameachiwa kama urithi
na wazazi wake. Akafikiria jinsi ambavyo njaa inamsumbua hana mbele wala nyuma,
msaada hapati. Hasira zikamwijia, hapo akaona atoke na kwenda kuzurura walau
aipoze njaa ama akajaribu kutafuta namna ya kuitoa.
Katika pitapita
zake ndani ya mitaa, aliweza kupita karibu na sehemu moja ambapo kunauzwa pombe
za kienyeji, akiendelea na safari, mara alisikia maongezi ya walevi ambayo
ingawa mwanzoni hakuyatilia maanani lakini baada ya kuyasikiliza kwa umakini
alijikuta akivutikanayo kwa kiasi fulani. Akatamani kusogea eneo lile ili walau
aweze kuyasikiliza kiundani zaidi.
‘’ Vitu kama vile
nyumba, viwanja... Sijui godoro, ni mambo ambayo huwa tunayanunua ili siku moja
yaweze kutufaa... Wewe vipi bwana! Hujui kama kuna siku maji yanaweza kukufika
shingoni ukapatwa na tatizo halafu kiwanja ama nyumba uliyojenga vikawa msaada
kwako?’’
‘’ Nyumba na
viwanja ni msaada kwa wanangu na si kwangu bwana. Hebu usiniletee.’’
‘’ Ah! Wewe nd’o hamnazo kabisa. Ina maana upo
radhi ufe njaa ilhali nyumbani una nyuma na kiwanja? Unashindwa vipi kuuza
sasa. Wewe uza iliupate pesa ya chakula. Usikubali kufa wakati yumbani kwako un
a nyumba bwana.’’
‘’ Ila kweli. Ukifa
na njaa, nyumba utamwachia nani? Nimekwelewa binamu... Hebu mwambie Maua
aongeze gongo hapa tunywe.’’
Ingawa mada ya
walevi wale ilibadilika lakini yeye kuna jambo ambalo lilimwijia ndani ya akili
zake. Akajikuta akishughulishwa na jambo lile, huku kichwani akiitafakari
nyumba yao ambayo kwake haioni faida yoyote, lakini pia aliifikiria njaa
iliyokuwa ikiusokota utumbo wake. Hapo akazidi kuchoka zaidi na zaidi.
Siku hiyo alijitahidi
walau kuombaomba mtaani lakini hakuna binadamu aliyonesha kumjali. Kila mmoja
alikuwa na matatizo yake wala asifikiri kuhusu yeye. Kijana yule njaa ikiwa
imemzidi zaidi, aliamua kurejea nyumbani kwake kwa hasira na kwenda hadi
kitandani kisha kilio cha uchungu kikamfika.
Alilia sana, lakini
kulia kwake hakukuwa njia ya kuiondoa njaa aliyokuwanayo. Hapo ndipo mawazo ya
walevi yalipomrejea kwa mara nyingine. Akautumia muda wake kuyatafakari mawazo
yale kwa umakini yeye mwenyewe huku akiiomba njaa yake ushauri.
‘’ Kati ya nyumba
na chakula bora nini?’’ alijiuliza. Majibu yalikuja ndani ya kichwa chake na
hapo akaamua. ‘’ Nauza nyumba niloachiwa na wazazi wangu. Ilimradi nisife
njaa.’’
Hatimae Mtoto yule
aliibuka na suluhisho la namna ile, hapo sasa usingizi wa amani ukamwijia.
Akalala usiku ule kwa raha mustarehe huku akitamani paweze kukucha iliatafute
mteja ataeweza kununua nyumba ile.
***
Siku
iliyofuata, mtoto Maduhu akiwa kama mmiliki halali wa nyumba ile aliyoachiwa na
wazazi wake. Hakuhitaji ushauri kutoka kwa yeyote aliyemzidi umri. Alitangaza
mnada wa nyumba ile ambayo nd’o urithi wa pekee alioachiwa na wazazi wake.
Kipindi cha nyuma baba Maduhu alipopata kiasi fulani cha pesa, aliamua kununua
kiwanja na kujenga nyumba ile kwa ajili ya yeye na familia yake waweze
kujistiri lakini leo hii mwanae shida zimemjaa na kuona njia pekee ya kutatua
matatizo yake ni kuuza nyumba. Mshauri mkuu akiwa ni tumbo lake.
ITAENDELEA.
0 comments:
Post a Comment