IMELETWA KWAKO NA SIMULIZI MIX ENTERTAINMENT
MWANDISHI: FRANK MASAI
SEHEMU YA TATU
ILIPOISHIA
"Beda. Muondoe
misuti yake huyu bwana." Mzee Pujini alimsukumia Lobo kwa Beda, jamaa
fulani wa makamo na kwenye mwili mkubwa kutokana na kunyanyua vitu vizito.
Naye Beda bila kuchelewa,
akaanza kumwondoa nguo John Lobo na wakati huo Lisa na Mubah walishatoka katika
chumba kile na Mzee Pujini alishakifunga.
ENDELEA
****
"Lobo. Nia yako na
washirika wako ni nini?" Sauti ya kiume ilisikika katika chumba kiitwacho
123F6. Ilikuwa ni sauti ya Malocha
ikitoka kwenye spika zilizopo kwenye chumba kile.
Lobo alikuwa akivuja damu
nyingi kifuani na maeneo ya usoni. Alikuwa kalegea kwa mateso makali ambayo
yalitoka mikononi mwa Beda na Mzee Pujini.
"Kazi yangu ni kuuza
au kununua roho tu! Sina kazi nyingine. Sina nia na wala sijui washirika wangu
ni wakina nani." Lobo alijibu swali la Malocha na baada ya jibu hilo,
Malocha alitoa ruhusa ya mateso kuendelea.
Mzee Pujini akachukua
kile kibubu chenye gesi na kuwasha gesi ile. Baada ya kuweka moto fulani kwenye
kibubu kile cha gesi, akamfata Lobo na kuanza kumpitishia machoni bila kumdhuru
bali kumsikilizisha joto litokalo mle kwenye kibubu.
"Joto hili linaenda
kwenye maungo yako ya uzazi." Mzee Pujini akiwa kavalia kama Daktari,
akaongea huku taratibu akianza kushusha moto ule kwenye maeneo ambayo kayataja.
Licha ya hayo yote
kutukia, uso wa John Lobo ulikuwa si wenye mashaka wala uoga. Ni kama
alishazoea yale mateso, lakini yote ni sababu alikuwa mkomavu katika nyanja
kama zile.
Mzee Pujini akafika
maeneo ya uzazi ya John Lobo, na bila kusita akapulizia gesi ya moto maeneo
yale na kumfanya John Lobo atoe sauti kali iliyochanganyika na maumivu. Hakika
mkomavu na kamanda wa mateso, alikuwa anaumia.
"You fu**n,
motherfu***r you're hurting me. (We mpumbavu, (tusi). Unaniumiza)." Sauti
ya maumivu makali ilisikika kutoka kwenye kinywa cha Lobo ikifuatana na matusi
mazito ya wazazi kumuelekea Mzee Pujini.
"Sema ukweli tuache
hili zoezi." Mzee Pujini aliacha kuchoka maeneo nyeti ya Lobo na kumuomba
aseme ukweli.
"Pale
nitakapofanikiwa kusimama kwenye hiki kiti, wewe ndio utakuwa wa kwanza
kufa." John Lobo alimwambia Mzee Pujini maneno ambayo yule mzee
alitabasamu kwa dharau kisha akaangalia kile kioo ambacho wa ndani hamuoni wa
nje ikiwa ni ishara ya kuwaambia waulize swali lingine.
"Lobo. Hatupo hapa
kukuumiza. Ni rahisi tu! Unashirikiana na nani na nini nia yako kwa
ufanyayo." Swali lilelile lilitoka kwenye kinywa cha Malocha.
"Hahahaaa. Malocha,
mbona unajiumiza sana. Nimekwisha kwambia, sina nia zaidi ya kuuza na kununua
roho za watu. Au unataka nikwambie duka la roho lilipo?" Lobo aliuliza
huku uso wake ukielekea kwenye kile kioo kana kwamba anawaona wale wanaomtupia
maswali kwa kunong'onezana.
"Lobo. Hatupo katika
utani. Umemuua Kamanda wa Kikosi cha Upepelezi kanda ya kati. Umewatishia amani
mawaziri mbalimbali na kauli yako ya kununua roho zao. Ukawaua baadhi ya
viongozi hao. Ukaona haitoshi, ukaanza kuwaondoa mabalozi mbalimbali wa nchi
hii kwa kuwaua. Sasa umegusa pabaya zaidi. Marekani. Umegusa nchi ambayo
hatuiwezi kwa kitu chochote....." Sauti ya Malocha ilikuwa ikielezea
baadhi ya maovu ya John Lobo lakini kabla hajamaliza maongezi yake, sauti yenye
hasira kupindukia, ilimkata kauli.
"Eti hatuiwezi kwa
chochote. Ni ujinga gani ambao umekujaa kichwani we' mpumbavu? Marekani
anachotuweza ni nini? Au ndio kasumba zenu za uoga bado zimewatawala kichwani
mwenu? Huyu Frank anapambana na
kutafutwa kwa udi na uvumba na watu gani? Si ni hawahawa Wamarekani? Mbona
hawampati? Mbona hata wakimpata wanamshindwa? Kaua makomando wangapi
Wakimarekani. Usiwe mjinga Malocha. Umiza kichwa fala wewe." Kauli chafu
zilitiririka toka kinywani mwa Lobo na hakuna aliyethubutu kumkatiza hadi
alipomaliza mwenyewe.
"Sound like it's
true. But none of it is real. (Sauti kama ya ukweli. Lakini hakuna kati hivyo
chenye uhalisia)." Malocha aliongea kwa kutumia lugha ya ughaibuni.
"Frank, never killed any commander from America. He just killed the
terrorists, and bad guys. (Frank hakuua kamanda yeyote wa Kimarekani. Aliua
wavamizi na watu wabaya pekee)." Sauti ya Lisa iliunga maelezo ambayo
Malocha aliyaacha kati.
"Inaonekana hamjui
lolote la kwa nini Frank anatafutwa na kwa nini kajificha. Na mbaya zaidi, hao
anaowaua ndio mimi na baadhi yenu nyie wapelelezi mnawasujudia. Mtakufa kama
panya kwenye sumu kwa mkono wangu." Lobo aliongea kwa hasira huku
akijaribu kuchomoa mikono yake toka kwenye kiti alichokuwa kafungwa barabara na
wazee wa kazi wa chumba 123F6. Hali ya
kujikakamua ili atoke pale kwenye kiti, ilifanya mwili wake ututumke na
kusambaa misuli kama ananyanyua vitu vizito.
"Mzee Pujini. Fanya
yako." Malocha aliongea kumruhusu tena Mzee Pujini aendeleze adhabu zake.
Mzee Pujini naye bila kusita, akajaribu moto wake angani kabla hajaanza kazi ya
kuchoma ngozi nyeusi ya John Lobo. **** "Hahahahahaa. Kuna muda hamna haja
ya kulia bali kucheka kwa sababu maumivu uyapatayo, ni sawa na kukutekenya
tu." Sauti ya John Lobo iliongea baada ya Mzee Pujini kumaliza kumchoma
kwa gesi maeneo ya ndani ya mapaja na kifuani.
"Look like you are
so tough. Lets see. (Unaonekana kama mgumu. Ngoja tuone)." Sauti ya Beda,
mshirika au msaidizi wa Mzee Pujini ilisikika ikiongea hayo huku ye' mwenyewe
akivaa grovu tayari kutimiza majukumu yake.
Beda akachukua visu
fulani vidogo vilivyo kwenye mkoba maalumu kwa ajili ya kuvihifahidhia. Na
baada ya kukamata visu hivyo viwili, akawa anavinoa kwa kuvisugulisha vyenyewe
kwa vyenyewe huku akitembea mbele ya Lobo huku na huko.
Visu vilivyokuwa
vinang'aa kama almasi lakini ni vya siliva, vilipita kifuani mwa Lobo haraka na
kuacha alama kama ya X kifuani hapo, na kabla hata Lobo hajalia kwa sababu ya
maumivu, akamwagiwa mafuta fulani spesheli ambayo yanauma si kawaida pale
yawekwapo kwenye vidonda, lakini ni tiba tosha kwa ambaye anavuja damu.
"Fuc*** you FISSA.
And fuc** you all and your mama."Lobo alitukana matusi mazito ya
Kimarekani kwa sababu ya maumivu makali yaliyokuwa yanampata kwa wakati ule.
Hakika alikuwa katika mateso, lakini bado hakuwa tayari kusema ukweli wowote.
"Lobo. Nia yako ni
nini na washirika wako ni wakina nani?" Malocha aliuliza kwa sauti kali
tena.
"Nia yangu ni
kusafisha pasafi kwa kuweka uchafu. Washirika wangu ni uchafu,
umenielewa?." Lobo alijibu kwa hasira kali zilizokuwa zimemjaa moyoni
sababu ya kuchanjwa na kuteswa na FISSA.
"Mkuu, niachie mimi
nikamuhoji mlemle." Mubarak alitoa ombi ambalo halikukataliwa kwa sababu
majibu ya John Lobo yalikuwa hayana mashiko hata kidogo vichwani mwao.
"Ooh! Mubah. Umekuja
kuchukua ujumbe wako." Lobo alitoa tabasamu pana baada ya kumuona Mubarak
kaingia ndani ya chumba kile.
Mubah hakuongea chochote
zaidi ya kuchukua chuma chenye ncha kali kwenye ule mkoba wa kuhifadhia vifaa
hivyo vya mateso.
"Nauliza swali.
Nataka jibu sahihi." Mubah alimwambia Lobo huku akikaa kwenye kiti ambacho
alikivutia mbele ya Lobo. Lobo badala ya kujibu, alitabasamu tena. Tabasamu la
kukereketa hata ubongo wa kichaa.
"Mubah. There's two
choices. Buy or Sell. (Mubah. Kuna machaguo mawili. Nunua au Uza)" Lobo
alimwambia Mubah kwa sauti tulivu. Mubah hakuwa mwenye wasiwasi bali kumtaza
John Lobo machoni."The rules of these choices are very simple. (Sheria za
haya machaguo ni marahisi sana)" Sauti ya Lobo ilizidi kuchukua
nafasi."Acha kazi yako au endelea na kazi yako. Ukiacha kazi, utakuwa
umenunua roho za familia yako. Watanusurika na mikono yangu. Ukiendelea na
kazi, utakuwa umeniuzia roho za uwapendao. Rahisi sana." Lobo alimaliza
kauli yake na hapohapo kwa hasira, Mubah alikandamiza kile chuma chenye ncha
kali kwenye paja la Lobo.
Kabla hata Lobo hajakaa
sawa kusikilizia yale maumivu, akapokea konde zito la shavu la kushoto hadi
damu zikaruka upande mwingine.
Tayari Mubah alikuwa
kapandwa na hasira kali ambazo zilimpelekea kusimama na kuanza kumpa mateke
mazito John Lobo. Hata pale Malocha alipomuamuru aache anachokifanya, hakusikia
lolote bali ngumi na mateke ndivyo aliona ni suluhu tosha kumpunguzia hasira.
Ni Beda na Mzee Pujini
ndio walimkamata na kumsogeza pembeni asiendelee kufanya 'unyambirisi' aliokuwa
anaufanya. Kiti alichokuwa kakalishwa
Lobo, kilikuwa kimechimbiwa chini hivyo wakati anapigwa alikuwa hadondoki wala
kuyumba, hivyo kufanya maumivu kumwingia vilivyo.
"Fpuu." Lobo
alitema damu pembeni baada ya Mubah kuwa anasukumwa pembeni.
"Mtoeni nje."
Sauti ya kwenye spika ilisikika ikiamuru Mubah atolewe nje.
"Mubah." Lobo
alimuita Mubah kabla hajatoka. Mubah akageuka kumuangalia yule mtu aliyemuita.
"Sijabadili maamuzi
yangu. Anza kuhesabu sasa, unamasaa ishirini na nne kufanya nilichokwambia.
Angalia saa yako, au angalia ile pale." Lobo alimuonesha kwa macho saa
iliyokuwa ukutani. Mubah akaiangalia kisha akarudisha macho yake kwa Lobo.
"Tick Tock."
Lobo aliongea sauti ya mshale wa saa na kumfanya Mubah ajikurupue toka kwenye
mikono ya Mzee Pujini na Beda kwa ajili ya.kwenda kumpa kisago tena Lobo.
Lakini hakufanikiwa hilo kwa sababu tayari alikuwa kwenye mikono imara.
"Unafanya nini
Mubah." Malocha alimuuliza kwa hasira Mubah baada ya kutolewa katika kile
chumba.
"Ni hasira mkuu.
Kaniambia maneno ya ajabu sana yule mjinga."
"Hasira za kijinga
hizo. Unadhani wakina Beda wangekuwa wanaendekeza hasira kwa kutukanwa na
kutishiwa, watuhimiwa wangekuwa wanapona?" Mubah akainamisha kichwa chini
na kujiona amekosa mbele ya Mkuu wake.
"Embu twendeni
ofisini." Malocha aliamrisha na hakuna aliyekataa kati ya Lisa na Mubah
ambao walikuwa kwenye kile kioo wakifatilia mateso ayapatayo Lobo kwa makini na
ukaribu.
BAADA YA NUSU SAA.
Ni king'ora kilichokuwepo
ndani ya Shirika lile la siri, ndicho kilichowashtua Lisa, Malocha na Mubah
waliokuwa ofisini wakijadili njia mbadala za kumfanya Lobo aongee.
Kabla hawajajua sababu ya
king'ora hicho kulia, mara mlango wa kioo wa ofisi ya Malocha, aliingia
mfanyakazi mmoja akiwa kavaa "headphones" masikioni zilizounganika na
kipaza sauti moja kwa moja. Ukimuona ni kama mtangazaiji wa radio fulani,
lakini sio.
"Mkuu. Lobo
katoroka. Na kawaua Beda na Mzee Pujini." Taarifa hizo zikawakurupua wale
vijana wa kazi kwa pamoja na kuanza kuelekea kule walipomuacha John Lobo.
Wakaingia moja kwa moja
kwenye kile chumba ambacho walimuacha Lobo, lakini macho yao yalitua kwenye
miili ya wachapa kazi wao ikiwa maiti, tena si maiti pekee, bali maiti za
kutisha.
ITAENDELEA
HUYO NDO JOHN LOBO ...USIKOSE SEHEMU YA NNE PAPA HAPA KUENDELEA KUSOMA CHECHE ZA HUYU JAMAA..
Simulizi Mix Entertainment We Touch Your Feelings
HUYO NDO JOHN LOBO ...USIKOSE SEHEMU YA NNE PAPA HAPA KUENDELEA KUSOMA CHECHE ZA HUYU JAMAA..
Simulizi Mix Entertainment We Touch Your Feelings
0 comments:
Post a Comment