Friday, July 7, 2017

DUKA LA ROHO SEHEMU YA SABA
IMELETWA KWAKO NA SIMULIZI MIX ENTERTAINMENT
MWANDISHI FRANK MASAI

ILIPOISHIA
"Nimekwisha kwambia, acha hiyo kesi. Ni amri siyo ombi. Nakupa miezi miwili ya kupumzika, utake usitake, utaenda mapumziko." Malocha ikabidi atumie nguvu za uongozi wake kuwasilisha hisia zake. Mubah akatulia kwa muda kabla hajarudi kwa yule opareta na kuchukua ule mkanda wenye tukio zima la siku hiyo.
ENDELEA
"Familia yangu ipo?" Mubah alimuuliza Malocha kabla hajachukua hatua nyingine kutoka mle ofisini.
"Nyumba na walinzi wakiwa na familia yako, vyote vilipigwa kiberiti. Hakuna ambacho kimesalia, labda majivu." Malocha alimjibu Mubah huku uso wake akiutazamisha mbele na chozi la kiume likamtiririka jasiri huyu upande wake wa kulia.
"We will be fine boss. Don't cry sir (Tutakuwa sawa mkuu. Usilie)" Mubah akamwambia mkuu wake huku akimgonga gonga bega lake kumfariji. Baada ya hapo, akatoka nje ya ofisi ile na kuelekea kwa Lisa ambaye baada ya kumuona Mubah, alimkimbilia na kumkumbatia.
"Upo sawa Mubah." Lisa alimuuliza baada ya kumuachia.
"Nipo sawa Lisa. Lakini bado sijajua ni vipi Lobo alijua kuwa familia yangu ipo kule." Mubah alimuuliza Lisa.
"Nadhani kuna kitu alikiacha katika mwili wa mwanafamilia wako, hicho ndio kilikuwa na GPS ambayo inaonesha popote waendapo." Lisa akamjibu Mubah na hapo Mubah akakumbuka kile kibanio kilichokuwa kina sumu hatari kutoka kwenye Yellowstone. Lakini pia akakumbuka maneno ya mjomba wake kuwa alipewa kibanio na kitu kingine ambacho yule mjomba hakumalizia kukisema baada ya Mubah kumpora kile kibanio.
"Nadhani itakuwa hivyo maana kuna sumu waliivuta wale wenzangu wengine, ilitoka kwenye banio ambalo mimi nilimpora Husna, mjomba wangu. Lakini pia Husna alipewa kitu kingine na Lobo, nadhani kiliambatana na hiyo GPS. Ila hamna tatizo, naenda likizo ya miezi miwili, lakini sitalala. Nitakutumia sana kukupa taarifa za kila upelelezi wangu." Mubah alimwambia Lisa na kisha wakaongea maneno machache ya kufarijiana kabla Mubah hajachukua jukumu la kwenda chumba cha mapumziko kilichomo FISSA.  **** "Bado sijaipata mkuu. Na familia yote ya Prince Mubarak imeteketea." Ni sauti ya Malocha ikiwa inaongea kwenye simu ambayo ilipigwa usiku ule wa saa tano. Alikuwa rais wa nchi akiulizia ndege kama imepatikana.
"Nasemaje. Mi' sijali hayo mambo yenu ya kijinga kwenda kukamata mtu mmoja kwa kutumia watu mia badala ya kufata maelezo ya mtu anachokitaka. Nachotaka mimi hapo ni hiyo ndege tu! Jumamosi ijayo Rais wa Cuba anakuja, unadhani kuna nini kitatokea kama hiyo ndege haijapatikana? Naitaka hiyo ndege kabla ya Jumamosi." Rais akakata simu na kumuacha Malocha akiwa katika wakati mgumu kuliko nyakati zote ambazo kawahi kuzipitia kimaongezi.
Akiwa na hasira za kuweza kufanya jambo lolote bila kujizuia, akatoka nje ya ofisi yake na kisha akaita wafanyakazi wote wa lile shirika.
"Ondokeni wote usiku huu. Sitaki mtu humu." Malocha aliongea kwa hasira baada ya mjumuiko wa wafanyakazi wake kuja eneo husika.
"Lakini mkuu, si ruhusa kuondoka usiku." Mfanyakazi mmoja alikumbusha sheria ya shirika lao.
"Ninekwishasema. Lawama zote nitabeba mimi, na si yeyote humu. Poteeni haraka kabla sijafanya kitu cha ajabu humu." Walimjua Malocha vilivyo, hivyo baada ya kauli ile, wakazima vitendea kazi vyao na kwenda kwenye usafiri maalumu kwa ajili ya kuwatoa nje ya shirika lile.
Sasa shirika lote la kipelelezi likawa limebaki patupu. Hakuna mtu zaidi ya Malocha aliyekuwa analanda huku na huko akijaribu kutafakari hili na lile kuhusu John Lobo.
"Kanishinda huyu mbwa. Sina jinsi, inabidi nimtafute tu! Nadhani nitafanikiwa." Yalikuwa maneno ya Malocha akiongea peke yake. Baada ya maneno hayo, akaenda moja kwa moja ofisini kwake na kutwaa simu ya mezani, kisha akaifungua na kuweka kitu fulani ambacho kilisaidia watu wasinase maongezi ambayo watakuwa wanayaongea kupitia simu hiyo.
"Halo kaka." Malocha aliitika baada ya simu kupokelewa.
"Vipi Malocha." Jamaa wa upande wa pili alisalimia.
"John Lobo karudi." Malocha alimwambia yule jamaa wa pili.
"Mkamateni sasa." Jamaa akajibu kifupi na kukata simu. Malocha akapagawa kwa kitendo kile cha jamaa. Hakujua atafanya nini ili kumshawishi yule jamaa amsikilize.
Akatulia kwenye kiti chake akitafakari njia za kumvuta mtu wake amsikilize. Baada ya dakika kadhaa, akapata wazo la cha kufanya. Akatwaa simu yake tena na kupiga namba zilezile.
"Usinipigie tena Malocha." Jamaa alisikika akilalamika kwenye simu.
"Lisa yupo katika hatari ya kuuawa na Lobo." Malocha akaongea kwa kifupi na kisha akakata simu. *****
NYUMBANI KWA LISA.
Alifika mida ya usiku sana na kukuta aishio nao wamekwishalala. Akafungua mlango wa nyumba yake kwa funguo ambazo anazo na kisha akaingia chumbani kwake ambapo alivua mavazi yake ya kazi na kuyaweka pembeni. Akavaa mavazi ya kwenda kuogea na baada ya hapo akaelekea bafuni kujisafi.
Dakika saba za kujisafi zikatimia, ndipo akatoka akijipukuta na kuelekea katika kitanda ambacho analala na mume wake Bwana Gunner, jamaa mwenye asili ya Kameruni na Kirusi.  Lisa akavuta kipande cha shuka alichojifunika mumewe na yeye akajifunika tayari kwa kuutafuta usingizi.
"Kazi zako vipi. Na leo mbona usiku?" Gunner alimuuliza mkewe Lisa.
"Kuna matatizo makubwa ofisini." Lisa alijibu kimkato na kutulia kabla ya kushtuliwa na mkono wa Gunner uliopita kiunoni kwake na kumgeuzia upande wake. Wakawa wanabadilishana pumzi kwa sababu sasa walitazamana.
"Kumetokea nini?" Gunner akamuuliza Lisa swali ambalo Lisa alilijibu pia kwa kifupi lakini lilieleza kila kitu ambacho kilitokea.
Baada ya maelezo hayo, Gunner alimbusu Lisa mdomoni na Lisa naye hakuwa nyuma bali kumpa ulimi kabisa bwana yule mweusi na aliyejengeka mwili sababu ya mazoezi ayafanyayo.
Baada ya dakika tano, ni sauti za raha ambazo zilitawala mle ndani. Mabusu motomoto aliyokuwa anayatoa Gunner kwenda kwa Lisa, hakika yalifaa kuitwa pole yenye raha kwa Lisa. Mtoto wa kike akawa hoi kabla hata ya mshikemshike wa mapenzi kuanza.
Gunner akazidi kuonesha utundu wake kwenye mwili wa Lisa. Akabusu la kupitisha ulimi wake huku na huko hadi pale alipohakikisha mwili wa Lisa upo tepetepe na hoi kwa mambo mazito ambayo si rahisi kwa msichana wa kileo kuyapokea kwa mwanaume wake. Gunner akampa mtoto wa kike ile thamani ya ndoa yake, akampa kile ambacho kiukweli huzidisha hamu ya wapenzi kuwa pamoja. Na zaidi, huongeza chachu ya penzi.
Lisa akajikuta mwenye faraja mpya baada ya shughuli nzima aliyoifanya mumewe.
Na shughuli kama hiyo ndio hasa iliyomfanya Lisa asimfiche mumewe ambaye alikuja katika wakati mgumu alioupitia Lisa. Wakati ambao Lisa alikuwa hana msaada kifikra zaidi ya maumivu tele baada ya kupotea kwa kipenzi chake Frank Masai na wakati huo anasumbuliwa na baba yake akiyegundua ujauzito wake.

MIAKA KADHAA NYUMA.
"Lisa. Tumbo lako limebarikiwa kuliko wanawake wote katika dunia hii. We' ndiye thamani ya moyo wangu. Hakuna Frank bila Lisa na Lisa bila Frank." Ni sauti ya Frank ikiwa kitandani pamoja na Lisa ambaye Frank alikuwa akilipapasa tumbo lake.
"Naupenda sana ulimi wako Man'Sai. Kila mara hunipa faraja ya masikio yangu na kinywa changu." Lisa akamjibu Frank kwa sauti ya mahaba na kumuongezea busu zito lililoenda sambamba na kumbate la kushiba.
"Lisa. Nahitaji tumbo hili libebe kiumbe changu. Upo tayari?" Frank alimuuliza Lisa baada ya muda mchache wa kumaliza mahaba yao.
"Nakukaribisha Man'Sai. Sitajutia maamuzi yangu. We' ndiye kila kitu." Maneno hayo yalimtoka Lisa akiwa kitandani kwa Frank kipindi wapo chuo kikuu mwaka wa kwanza.  Mapenzi yao yalianza tangu sekondari na muda huo yalikuwa yameshamiri kama maua yaonayo asubuhi au ndege wa anga wasonapo jua limechomoza.
"Asante Lisa. Nategemea mwaka wa tatu tutatimiza ndoto hii." Frank akaweka nyongeza katika maongezi yao.
"Anytime Man'Sai."
"Thank you dear." Baada ya maneno hayo, purukushani za mahaba zikapamba moto tena na kufanya kitanda cha Frank kulalamika kwa kile kinachoendelea. ****
MIAKA MIWILI MBELE.

Ikiwa ndio wanamaliza chuo, kama kawaida ya Frank na Lisa, wakakutana kimapenzi zaidi lakini wakati huu walikuwa wanalengo la kusaka mtoto tu! Wiki hiyo wakawa wanakutana kimwili kila pale walipohitajiana. Lisa akiwa anajua wazi ndani ya wiki hizo ndipo awezapo kupata ujauzito, akawa haishi miguu yake kwa Frank. Na Frank alionesha urijali wake kwenye maeneo ya kitandani. Akawa mtu wa kutoa raha kwenda kwa Lisa na Lisa akitoa raha hizo kwenda kwa Frank.
Baada ya wiki mbili wakahitimu chuo kikuu. Huo ndio ukawa mwisho wa Frank na Lisa kuonana. Baba yake Lisa ambaye ni Gavana wa jimbo fulani huko Marekani, akamchukua Lisa kwa ombi la Rais wa nchi, na kumpeleka chuo cha mafunzo ya Ujasusi. Huko ndipo ambapo Lisa alipata wasaha wa kujifunza mbinu mbalimbali za kipelelezi na ujasusi.
Lakini kabla ya kuingia katika chuo hicho, ilibidi apimwe kwanza afya yake. Hapo ndipo alipogundulika anaujauzito wa mwezi mmoja. Baba wa Lisa, Mzee Lindsay, aliumia sana kwa kitendo kile. Ili kuficha aibu ile, akaamua kumtafutia mwanaume mtoto wake amuoe akiwa na mimba ile.
GUNNER SAMUEL BOKWA. Kijana mpole na mtulivu katika mambo yake. Anamiliki biashara kadhaa nchini Marekani, Ufaransa, Urusi na Kameruni alipotokea marehemu baba yake ambaye ndiye aliyemuachia urithi wa mali zote hizo. Siku zote katika maisha yake alikuwa ni mtu wa kumsumbua Mzee Lindsay kuhusu mtoto wake. Na baada ya baba wa Lisa kugundua mwanawake anamimba, akamkimbilia Gunner bila yeye kujua na kumuomba amuoe mwanaye kabla hajaenda chuo cha ujasusi. Gunner hakuwa na kipingamizi chochote kwa sababu mapenzi ni upofu. Akamfata Lisa ambaye tumbo lake bado lilikuwa halijaanza kuchipuka bali uzuri wake ulizidi maradufu.
Gunner akawa boya na bwege kabisa hasa pale alipopewa ruhusa ya kusadifu umbo mwanana la Lisa likiwa halina mavazi. Akalichezea wiki nzima kwa mahaba mazito. Mwisho wa yote ukawa ni harusi kubwa kufungwa katika jiji la Dar es Salaam. Lisa alijitahidi kuonesha furaha yake, lakini ukweli ni kwamba, hakuwa na furaha hiyo hasa baada ya kusikia mkasa ambao Frank na Malocha umewakumba kipindi hicho. Mkasa wa Jina la Chude Bobo. Walikuwa wanatafutwa kama dhahabu machimboni.

ITAENDELEA

KWENDA SEHEMU YA NANE BOFYA HAPA>> SEHEMU YA NANE

0 comments:

Post a Comment