DUKA LA ROHO SEHEMU YA TISA
IMELETWA KWAKO NA SIMULIZI MIX ENTERTAINMENT
MWANDISHI FRANK MASAI
ILIPOISHIA
"Hamna tatizo. Ila ni kibanio ghali sana kile, hadi nimeshtuka." Mubah alidanganya lakini ukweli ni kwamba kile kibanio alichokuwa nacho Martina, ndicho ambacho mjomba wake alipewa na Lobo. Yaani vinafanana. Ndicho kile kilichotoa sumu hatari kutoka kwenye Yellowstone.
ENDELEA
Wakarudi kwenye gari
baada ya maongezi machache na kisha gari likakaza mwendo kuelekea Kivule.
Kichwa cha Mubah
hakikutulia hata kidogo kimawazo. Akiwa katika mawazo hayo, ndipo akakumbuka
sura ile iliyompita kwenye gari wakati yeye anazimia. Akakurupuka tena na
kumuangalia Lisa kwa macho ya kushuku kitu. Lisa akabaki mwenye mshangao wa
hali ya juu kwa matendo nadra ayafanyayo Mubah.
"Yule ni Gunner,
mume wa Lisa. Mshenzi anashirikiana na Lobo. Mungu wangu." Mubah
akajisemea mwenyewe moyoni huku akimkodolea macho makali Lisa.
"We' Mubah
unamatatizo gani!? Hiyo tabia umeitoa wapi." Ikabidi Lisa amuulize Muhah
jambo linalomsibu hasa baada ya kuona macho ya Mubah hayakauki usoni pake.
"Hakuna Madam. Basi
tu!" Mubah alijichekesha huku akijaribu kuumba tabasamu la mbao usoni
pake.
"Usinifanye mimi
mtoto Mubah. Mi' ni Jasusi na pia ni mpelelezi kuliko wewe. Najua unafahamu
kitu, haya haraka eleza nini kipo nyuma ya pazia." Lisa akauliza tena
akiwa katika uso usio na masikhara. Wakati huo, gari lao lilikuwa likizidi
kusonga mbele na Martina akionekana kufurahia mwenendo mzima wa safari ile.
"Hamna kitu madam
Lisa. Nitakwambia tukifika kwani kwa sasa kidogo, itafanya kazi yetu
kugoma." Mubah alijitetea huku akijing'ata ng'ata bila kujua sababu ya
kufanya hivyo.
"Basi sitaki
unitazame tena usoni. Acha kabisa." Lisa alifoka na kumuangalia mtoto wake
ambaye alikuwa anacheza kwa kumrusha mdoli fulani aliyenunuliwa na mama yake.
Mubah akaamua kutulia
kama si yule wa mwanzo. Na kwa bahati mbaya au nzuri, alikuwa anajali kazi
zaidi kuliko matukio yaliyompata. Akili yake yote ilijaa kisasi kuliko jambo
lolote lile. Gari ikazidi kutitia kwa
mwendo wa madaha hasa kwa sababu ya barabara mbovu ya kuelekea Kivule.
"Mama, baba
ananifundishaga kupiga kwa kutumia hiyo." Martina alimwambia mama yake
huku akisonta kidole kwenye kiuno cha dereva wa gari lile. Alikuwa kapachika bastola yake ambayo
ilionekana vema baada ya shati lake kujivuta na hiyo ndio ikampa wasaa Martina
kuongea hayo.
"Anakulengeshaga
nini?" Mubah alimuuliza Martina kwa hamasa huku Lisa akiwa kama haamini
kile ambacho anakisikia.
"Anakunywagwa bia,
halafu ananiwekea chupa nilenge. Siku nyingine ananipeleka porini na kuniwekea
mbao zikizochongwa kama watu, ananiambia niwe nawapiga kichwani au kifuani. Hao
ni maadui." Mtoto Martina alizidi kutiririka bila uoga.
"Na kingine
anachokufanyiaga." Mubah akatupa swali lingine.
"Ananipaga picha na
kuniambia huyo ni adui yetu, nikimuona kama nina bunduki nimpige
kichwani."
"Picha hiyo yupo
nani?"
"Mubah muache
mwanangu. Nitashuka sasa hivi. Sitaki huo ujinga kuusikia ukimuuliza
mwanangu." Ikabidi Lisa amfokee Mubah kwa sababu ya maswali makavu
amuulizayo mtoto wake wa pekee. Mubah
akameza mate ya hasira lakini akakaa kimya kwa sababu angeendelea, angemkosa
Lisa katika mipango yao. Kimya kikachukua nafasi yake na safari ya kwenda
Kivule ndio ilikuwa inaendelea kwa wakati huo. **** Malocha alikuwa hajui cha
kufanya baada ya kuisubiri simu ya jamaa aliyemtegemea labda atapiga baada ya
kusikia kuwa hata Lisa atakuwa matatizoni. Akawa amechoka kuisubiri kwa sababu
jamaa hakupiga wala kubipu au kutuma meseji.
Usiku wa manane Malocha
akawa analanda landa ndani ya FISSA bila kujua ni nini anatafuta au nini
anataka kufanya. Mara anaenda huku mara huko ili mradi awe anatembea tu.
Mwisho wake ulikuwa ni
ofisini kwake na mawazo tele yakimwandama hasa kwa sababu ya mtu wake kutopiga
wala kuitikia anachokitaka.
"Ina maana Masai
amekwisha sahau ahadi yetu? Kasahau kabisa kuwa nitakapomuhitaji nitamtaarifu?
Lakini hilo si kitu, inamaana pia kamsahau Lisa? Kamsahau kabisa mtu aliyesema
anampenda kila mara. Frank atakuwa anamatatizo huyu mtu." Malocha
alijisemea peke yake muda wa saa kumi usiku.
Ama kwa hakika alikuwa kapagawa hasa kwa matendo kama kuwafukuza
wafanyakazi wake wote usiku huo.
Asubuhi ya saa moja,
akiwa kidogo kapitiwa na usingizi, simu ya ofisini kwake ililia kwa nguvu na
kumfanya akurupuke kama mwenye kuwehuka. Alipoangalia kioo kodogo cha simu ile
ya mezani, aliona ni namba ya Ikulu ndio yenye kupiga.
"It's over now.
(Yameisha sasa)" Malocha aliongea hayo wakati akiiangalia simu hiyo
ikiita.
"Hallow mkuu."
Malocha aliita kwa sauti ya taratibu.
"Sijawahi kuona mtu
mpumbavu kama wewe. Jinga la kutupwa kama mbwa lililokosa matunzo. Yaani
unadiriki kufukuza wafanyakazi wote usiku kama vile shirika ni lako. Unavunja
sheria za shirika kama vile umelianzisha wewe." Rais alikuwa anaongea kwa
sauti ya juu kana kwamba alikuwa anaongea na mtu wa maili kadhaa mbali.
"Kwa hiyo unataka
nini mkuu. Nimeshafanya." Malocha akamuuliza mkuu wake kwa nyodo.
"Unasemaje we mbwa?
Dharau umezianza lini? Sasa kwa taarifa yako, nimekwisha andaa uongozi mpya.
Wewe, na mbwa wenzako hao wawili, Mubarak na Lisa, wote mtakuwa nje ya FISSA.
Katafuteni pa kufanyia kazi, si hapo. Sihitaji washenzi tena." Maneno hayo
yakaenda sanjari na kukata simu. Malocha akatabasamu kisha akaanza kukusanya kilicho
chake kabla ya huo uongozi mpya haujafika. **** "Usafiri uwatoao nje
wafanyakazi wa FISSA ni usafiri ambao si rahisi kwa mtu wa ndani kuona nje. Na
hata Malocha alipoamua kwenda kuupanda, ilikuwa ni vivyo hivyo.
Usafiri huu hutambua
sauti za wafanyakazi wote wa shirika lile la siri. Na pindi wapandapo, basi
hutoa sindano ndogo ambazo zinachomwa mikononi na usingizi mzito huwachukua
waliopanda usafiri huu. Pia hujiendesha wenyewe kwa kuwa umetengenezwa maalumu
kuwafikisha wafanyakazi wake sehemu husika.
Muda wa saa sita, Malocha
tayari alikuwa amekwishakwea kwenye usafiri mwingine ambao huo ulikuwa ni wa
wananchi wa kawaida. Wale wazoefu wa jiji na miji wanauita usafiri huu ni tax,
na ndio Malocha alikuwa kaupanda.
"Mkuu tunaelekea
wapi." Dereva mmoja mchangamfu alimuuliza mteja wake ambaye alikuwa kama
katoka kulewa pombe kali usiku wa jana.
"Nipeleke Kivule
Kamanda." Malocha alijibu na dereva yule hakujali gharama ambayo itatokea
kwa sababu muonekano wa Malocha, haukuwa wa kukosa fedha ambazo atamtajia.
"Hallow Mubah."
Malocha alisikika kwenye simu.
"Ndio mkuu."
"Hatuna chetu FISSA.
Fanya hima tukutane Kivule ukiwa na ripoti nzima ya Lobo."
"Sawa mkuu. Rais
ndio katutoa au?"
"Yaap. Ni
mkuu."
"Na nani mwingine
kamtoa."
"Lisa naye
katolewa."
"Okay. Basi na mimi
nakuja huko Kivule sasa hivi." Mubah aliongea kwa shahuku kubwa.
"Na mimi ndio nipo
Posta hapa, nakuja taratibu." Malocha akamalizia kabla ya kuanza maongezi
mengine ya kijamii na maisha na Mubah kupitia simu.
****
"Najua umeona hilo
bomu lilivoenda na kulipua nyumba yako. Lakini sasa unatakiwa kuangalia
mazingira ambayo bomu hilo limetokea. Rudisha huo mkanda nyuma na kuanza
kuchunguza kimoja baada ya kingine." Sauti ya Malocha ilikuwa ikimuelekeza
mtaalamu wa mmoja wa kompyuta aliyekuwa anacheza mkanda mzima ambao ulionesha
tukio zima lililotokea nyumbani kwa Mubah.
Nyumba hiyo ya Kivule,
ilikuwa ni nyumba moja kubwa kiasi na huwezi kujua ndani kunafanyika nini kama
hujaingia na kuchunguza.
Ndani ya nyumba hiyo
kulikuwa kumetapakaa dhana mbalimbali za Kijasusi na kipelelezi. Bunduki za
kila aina na vifaa vya kipelelezi, vilipendezesha chumba ambacho Mubah na
Malocha walisimama wakiwaangalia wale jamaa wanaocheza video nzima ya tukio la
Mubah.
"Hapo hapo Banchi.
Umeona hilo gari jeusi?" Mubah alimsimamisha jamaa mmojawapo wa kompyuta
na kumuonesha gari ambalo alilishuku vibaya. "Hilo ndilo nililiona wakati
nazimia. Naomba ulichunguze."
"Kama ndio hilo,
basi tutaanzia kazi zetu hapo. Cha msingi tupate namba za usajili za gari hili
(plate number)." Malocha aliongea huku kafumbata mikono yake kifuani.
"Namba hizi hapa
mkuu. Ni T 900 QJG." Opareta wa kompyuta zile, alitoa taarifa hizo na
kuwafanya Mubah na Malocha kusogea kwa karibu na kuzitazma.
"Okay. Safi Banchi.
Sasa Mubah, hapa tunamuhitaji sana Lisa kwa sababu yeye ni mwanamke awezaye
kuwavuta watu wowote na wakafungua vinywa vyao kusema siri. Cha msingi, mpigie
simu sasa hivi mwambie muonane Kitunda. Halafu mkikutana, mpe hii hapa simu
halafu ndio mje huku." Malocha alimpa maelekezo ambayo Mubah alikuwa
anatikisa kichwa kukubaliana nayo.
"Sasa kwa nini
unampa simu hii?" Mubah akamuuliza Malocha.
"Lisa yupo hatarini
bila yeye kujitambua. Mume wake si mtu kama anavyodhani, muda wowote anamgeuka.
Huyo ndio sababu ya Lobo kujua njia nyingi za FISSA kwa sababu anamuwekea GPS
kila anapojua zimetolewa. Nakwambia haya lakini usimwambie chochote kile.
Atakuja kuju a ya kumaliza mambo haya." Malocha alimuelekeza Mubah mambo
kadhaa, kisha kuanza kumpa siri za Lisa ambaye alikuwa anacheza na mwanaye anayesheherekea
siku yake ya kuzaliwa.
"Kwa hiyo mume wa
Lisa anashirikiana na Lobo."
ITAENDELEA
KWENDA SEHEMU YA KUMI BOFYA HAPA=> SEHEMU YA KUMI
ITAENDELEA
KWENDA SEHEMU YA KUMI BOFYA HAPA=> SEHEMU YA KUMI
0 comments:
Post a Comment